Ukubwa wa bofro……!!!!!!

Standard

Jamani miyemwenzenu pita pita yangu mitaa ya manzeshe  basi wacha nimuone jamaa mmoja mida ya saa sita mchana,kweupee hata bado hakuna kitu kiza,,huyo jamaa bonge  basi kakabana katoto kadogo kwenye ukuta,mwenzenu nkasema huyu jamaa ina maana haoni aibu kuibanananisha kile kitoto kidogo katikati ya barabara,japo kichochoroni lakini watu wanawaona bana halafu jamaa baunsa huyo.

Basi bwana waswahili wanakwambia kusutwa sio kazi ila kazi ukishikwa,,anyway tunaendelea na mada yetu,miye mwenzenu sikuwa na subira na roho ikanisokota kama rasta za mmasai kuona jamaa kakabananisha kabinti kale,,si nikaondoka nikaenda hadi pale kwa yule jamaa,nikamgusa bega,

He!! basi mwenzenu jamaa kugeuka na kunicheki,,hahahaahhah,,,jamani kumbe jamaa yule pale si riziki,na pale kile kibinti ni kishostito chake kilikuwa kinampa story za mabuzi jana yake waliyoyachuna maeneo ya magomeni,basi mwenzenu kuona hivyo  nikawa mdogo kama pilitoni,,hahaha kweli nimeamini ukubwa wa mkate kiboko yake chai

Leave a comment